Une militante congolaise violemment agressée à Mbarara en raison de son activisme

Par la DDH Birhahozagire Zihalirwa

La militante congolaise Furaha Bahati, connue pour son engagement constant en faveur de l’égalité des droits et de la justice sociale, a été violemment agressée dans la nuit du 15 février à son domicile situé dans la ville de Mbarara, en Ouganda.

Réfugiée congolaise depuis plusieurs années, Furaha Bahati vit en Ouganda après avoir fui les atrocités et les persécutions qu’elle aurait subies de la part de certains officiels du camp de réfugiés de Nakivale, en raison de son activisme et de ses prises de position en faveur des droits humains. Malgré son déplacement à Mbarara dans l’espoir de trouver sécurité et protection, elle demeure la cible de violences répétées.

Dans la nuit du 15 février, des assaillants ont fait irruption dans sa maison et l’ont brutalement tabassée, la laissant gravement blessée, avec du sang coulant sur son visage. Cette attaque est largement perçue comme une représaille directe liée à son engagement militant.

Le drame de Furaha Bahati s’inscrit dans une longue série de violences tragiques visant sa famille. Elle a déjà perdu son mari, Fidèle Rubondo, frappé et tué à Nakivale. Plus récemment, il y a quelques mois à peine, son fils Justin Rubondo a lui aussi été violemment agressé puis tué. Ces pertes successives illustrent un climat d’insécurité extrême et d’impunité persistante.

Comme si cela ne suffisait pas, dans la nuit d’hier, aux environs de 2 heures du matin, la maison de Furaha Bahati a de nouveau été saccagée, et elle a été violemment blessée lors de cette nouvelle attaque. Ces agressions répétées soulèvent de graves préoccupations quant à sa sécurité, ainsi qu’à celle des défenseurs et défenseures des droits humains vivant en exil.

Cette situation appelle une intervention urgente des autorités ougandaises, ainsi que l’attention des organisations internationales de défense des droits humains, afin que la sécurité de Furaha Bahati soit assurée, que les auteurs de ces violences soient identifiés et traduits en justice, et que cesse l’impunité dont bénéficient les agresseurs.

Le cas de Furaha Bahati est un rappel tragique des risques extrêmes auxquels sont exposés les militants des droits humains, en particulier les réfugiés, même en dehors des zones de conflit.

La version Swahili suit

Mwanaharakati wa Kongo ashambuliwa kikatili mjini Mbarara kwa sababu ya harakati zake

Mwanaharakati wa Kongo Furaha Bahati, anayejulikana sana kwa kujitolea kwake kwa miaka mingi katika kupigania usawa wa haki na haki ya kijamii, alishambuliwa kikatili usiku wa tarehe 15 Februari nyumbani kwake katika mji wa Mbarara, Uganda.

Akiwa ni mkimbizi wa Kongo kwa miaka kadhaa, Furaha Bahati anaishi Uganda baada ya kukimbia ukatili na mateso aliyodai kufanyiwa na baadhi ya maafisa wa kambi ya wakimbizi ya Nakivale, kutokana na harakati zake za kutetea haki za binadamu. Licha ya kuhamia Mbarara kwa matumaini ya kupata usalama na ulinzi, bado anaendelea kulengwa na mashambulizi ya mara kwa mara.

Usiku wa tarehe 15 Februari, washambuliaji waliivamia nyumba yake na kumpiga kikatili, wakimuacha akiwa amejeruhiwa vibaya, damu ikimtoka usoni. Shambulio hili linaonekana wazi kuwa ni kisasi kinachohusiana moja kwa moja na shughuli zake za kiharakati.

Msiba wa Furaha Bahati ni sehemu ya mlolongo mrefu wa vurugu zilizolenga familia yake. Tayari alipoteza mume wake, Fidèle Rubondo, ambaye alipigwa na kuuawa katika kambi ya Nakivale. Hivi karibuni pia, miezi michache iliyopita, mwanawe Justin Rubondo naye alipigwa na kuuawa. Vifo hivi vya mfululizo vinaonesha hali mbaya ya usalama na kuendelea kwa kutokuwajibika kwa wahusika.

Kana kwamba hayo hayatoshi, usiku wa jana majira ya saa nane usiku (saa 2:00 asubuhi), nyumba ya Furaha Bahati ilisakwa na kuharibiwa, na yeye mwenyewe alijeruhiwa vibaya tena katika shambulio jipya. Mashambulizi haya ya mara kwa mara yanazua wasiwasi mkubwa kuhusu usalama wake na wa watetezi wengine wa haki za binadamu wanaoishi uhamishoni.

Hali hii inahitaji hatua za haraka kutoka kwa mamlaka za Uganda, pamoja na kuhusisha mashirika ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu, ili kuhakikisha ulinzi wa Furaha Bahati, kuwabaini na kuwafikisha mbele ya sheria waliohusika na mashambulizi haya, na kukomesha hali ya kutokuchukuliwa hatua dhidi ya wahalifu.

Kisa cha Furaha Bahati ni ukumbusho wa kusikitisha wa hatari kubwa wanazokumbana nazo wanaharakati wa haki za binadamu, hasa wakimbizi, hata wanapokuwa mbali na maeneo ya migogoro.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top